Home » » SAMATTA AIPA USHINDI TP MAZEMBE KLABU BINGWA AFRIKA-FAINALI

SAMATTA AIPA USHINDI TP MAZEMBE KLABU BINGWA AFRIKA-FAINALI

MAZEMBE                                                                                                                                STRAIKA mahiri wa Tanzania Mbwana Samatta Jana Usiku alifunga Bao la ushindi kwa Klabu yake TP Mazembe ya Congo DR walipocheza Mechi ya Kwanza ya Fainali ya CAF CHAMPIONZ LIGI dihidi ya USM d’Alger huko Algiers na kushinda 2-1.
Bao hilo la Samatta lilifungwa kwa Penati katika ya Dakika ya 79.
TP Mazembe walitangulia kufunga Bao katika Dakika ya 27 kupitia Rainford Kalaba na Mchezaji huyo kutolewa kwa Kadi Nyekundu Dakika ya 45.
Nao USM d’Alger walibaki Mtu 10 kuanzia Dakika ya 67 baada ya Hocine El Orfi kutolewa nje kwa Kadi Nyekundu na Mazembe kupewa Penati ambayo Nathan Sinkala wa Zambia alikosa.
USM d’Alger walisawazisha katika Dakika ya 88 kwa Bao la Mohamed Sequer lakini Mtanzania Mbwana Samatta akaleta ushindi kwa Bao lake la Penati na TP Mazembe kuibuka kidedea kwa Bao 2-1.
Marudiano ya Fainali hii ni Novemba 8 huko Lubumbashi, Congo DR.
Mshindi wa Fainali hizi atazoa Donge la Dola Milioni 1.5 na pia ataiwakilisha Afrika kwenye Mashindano ya FIFA ya Klabu Bingwa Duniani huko Japan Mwezi Desemba.
CAF CHAMPIONZ LIGI
FAINALI
Ratiba/Matokeo:
**Saa za Bongo
Jumamosi Oktoba 31
Union Sportive Medina d’Alger [Algeria] 1 TP Mazembe [Congo, DR] 2
Marudiano
Jumapili Novemba 8
1630 TP Mazembe v Union Sportive Medina d’Alger
Toa maoni yako kwa habari hii kwa kuweka email yako hapa,na endelea kutufatilia zaidi Ukurasa wa habari

0 comments:

 
Supported by AMAGA Media services : | |
Copyright © 2015. UKURASA WA HABARI - All Rights Reserved
Templete Designed by Abdallah Magana
Proudly powered by Blogger