Home » » MOURINHO;KUBAKI CHELSEA LICHA VIPIGO MFULULIZO

MOURINHO;KUBAKI CHELSEA LICHA VIPIGO MFULULIZO

 MOURINHO-SHINGONI                                                                                                                                    MENEJA wa Chelsea Jose Mourinho atabakia kwenye kibarua chake kwa sasa licha ya Jana kutandikwa 3-1 Uwanjani kwao Stamford Bridge na Liverpool kwenye Mechi ya Ligi Kuu England ikiwa ni ni kipigo chao cha 6 katika Mechi 11 za Ligi hiyo Msimu huu.
Chelsea, ambao ndio Mabingwa Watetezi wa Ligi Kuu England, wapo Nafasi ya 15 kwenye Msimamo wa Ligi wakiwa Pointi 14 nyuma ya Vinara Man City.
Akihojiwa mara baada ya kipigo cha Jana kama anadhani hiyo ndio Mechi yake ya mwisho kama Meneja, Mourinho alijibu: “Hapana. Sifikirii hilo!”
Mourinho, ambae hajawahi kufungwa zaidi ya Mechi 6 za Ligi katika Msimu mmoja akiwa kama Meneja wa Chelsea, aliongeza: “Mapambano yanaendelea lakini wakati mwingine mapambano haya ni magumu kushinda. Unaingia kwenye mapigano na silaha nyingine!”
MATOKEO:
Jumamosi Oktoba 31
Chelsea 1 Liverpool 1       
Crystal Palace 0 Man United 0              
Man City 2 Norwich 1                
Newcastle 0 Stoke 0                  
Swansea 0 Arsenal 3        
Watford 2 West Ham 0               
West Brom 2 Leicester 3   
RATIBA:
**Saa za Bongo
Jumapili Novemba 1
1630 Everton v Sunderland                  
1900 Southampton v Bournemouth                 
Jumatatu Novemba 2
2300 Tottenham v Aston Villa
 BPL-STAND-OCT31
Toa maoni yako kwa habari hii kwa kuweka email yako hapa,na endelea kutufatilia zaidi Ukurasa wa habari

0 comments:

 
Supported by AMAGA Media services : | |
Copyright © 2015. UKURASA WA HABARI - All Rights Reserved
Templete Designed by Abdallah Magana
Proudly powered by Blogger