Magazeti ya Tanzania leo Novemba 11, 2015


.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
DSC02230
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
DSC02238
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.

BIG MECHI ZA KIRAFIKI IJUMAA HII SPAIN-ENGLAND, FRANCE-GERMANY.........

SPAIN-ENGLAND                                                                                                                                            BAADA LIGI KUBWA kwenda Vakesheni hadi Wikiendi ya Novemba 21, Wiki hii na mwanzo wa Wiki ijayo zipo Mechi kubwa nyingi za Kimataifa zikiwemo za kufuzu kucheza Fainali za Kombe la Dunia Mwaka 2018, kufuzu Fainali za EURO 2016 na nyingine ni za Kirafiki kwa Nchi zile ambazo hazipo kwenye michuano rasmi.
Mabara ya Marekani ya Kusini na Afrika yatakuwa kwenye Mechi za kusaka kucheza Fainali za Kombe la Dunia za Mwaka 2018 huko Russia wakati Barani Ulaya wana Mechi za Mchujo za kupata Timu 4 za mwisho kucheza Fainali za Mataifa ya Ulaya, EURO 2016, zitakazochezwa Mwakani huko France.
Katika baadhi ya Mechi za Kimataifa za Kirafiki ziko Bigi Mechi kadhaa kama vile Spain v England, France v Germany, Belgium v Italy, England v France, Belgium v Spain na Germany v Netherlands ambazo zitapigwa Ijumaa na Jumanne.
KIMATAIFA KIRAFIKI
Ratiba
*Saa za Bongo
Jumatano Novemba 11
15:00 Jordan v Malta                 
20:00 Estonia v Georgia             
Alhamisi Novemba 12         
17:00 Oman v New Zealand                 
19:00 Macedonia v Montenegro            
20:00 Andorra v Saint Kitts And Nevis            
Ijumaa Novemba 13        
3:00   Solomon Islands v Fiji                
20:30 Qatar v Turkey                 
21:00 Luxembourg v Greece                 
21:45 Poland v Iceland              
21:45 Northern Ireland v Latvia            
21:45 Belgium v Italy                 
21:45 Portugal v Russia              
22:30 Czech Republic v Serbia              
22:45 Spain v England               
22:45 Slovakia v Switzerland                
22:45 Wales v Netherlands                  
23:00 France v Germany            
Jumamosi Novemba 14         
10:00 Hong Kong v Macau
Jumanne Novemba 17
Tuesday 17 Nov 2015         
3:00   Italy v Poland                   
3:00   Lebanon v New Zealand              
14:00 Macedonia v Lebanon                 
18:00 Russia v Croatia               
19:00 Estonia v Saint Kitts And Nevis             
19:00 Azerbaijan v Moldova                 
20:15 Turkey v Greece               
21:30 Luxembourg v Portugal               
21:45 Austria v Switzerland                  
21:45 Poland v Czech Republic             
21:45 Slovakia v Iceland            
21:45 Belgium v Spain               
22:00 England v France              
22:45 Germany v Netherlands              
22:45 Italy v Romania      

MOYES AFUKUZWA KAZI REAL SOCIEDAD SIKU 1 TU KABLA KUTIMIZA MWAKA!

 MOYES-SOCIEDAD
                                                                                                                              David Moyes ametimuliwa kazi kama Meneja wa Klabu ya La Liga inayosuasua ya Real Sociedad ikiwa ni Siku 1 tu kabla hajatimiza Mwaka mmoja Klabuni hapo.

Moyes, mwenye Miaka 52, alitwaa wadhifa wa Umeneja wa Klabu hiyo ya Spain hapo Tarehe 10 Novemba 2014 na kuiokoa Klabu hiyo kuporomoka wakati ikiwa katika hali mbaya na kukamata Nafasi ya 12 kwenye La Liga Msimu uliopita.

Lakini Msimu huu mambo ni yale yale kwa Real Sociedad baada ya Ijumaa kuchapwa 2-0 na Las Palmas ikiwa ni kipigo cha 4 katika Mechi zao 5 zilizokwisha za La Liga.

Real Sociedad imetangaza Moyes na Msaidizi wake, Billy McKinlay, wote wamefukuzwa.

Kuhamia kwa Moyes huko Sociedad Mwaka Jana ilikuwa ni kibarua chake cha kwanza tangu atimuliwe Man United Mwezi Aprili 2014 baada ya kudumu Miezi 10 tu hapo Old Trafford.

Moyes, ambae kabla ya kutua Man United alikuwa Meneja wa Everton kwa Miaka 11, alikuwa ni Meneja wa 4 kutoka Uingereza katika Historia ya Real Sociedad.

Wengine waliomtangulia Klabuni hapo ni Harry Lowe alieingia Mwaka 1930 na kukaa Miaka 5, John Toshack alieiongoza Klabu hiyo kwa vipindi vitatu tofauti na cha mwisho kilikuwa Mwaka 2002 wakati Chris Coleman alikaa kwa Miezi 7 baada ya kuteuliwa Julai 2007.

Real Sociedad, ambao wako Nafasi ya 17 katika La Liga, watapambana na Sevilla, Mabingwa wa UEFA EUROPA LIGI, na kisha Barcelona, Mabingwa Watetezi wa La Liga na pia UEFA CHAMPIONZ LIGI, katika Mechi zao 2 za La Liga zifuatazo mara baada ya La Liga kurejea tena Wikiendi ya Novemba 21 baada kupisha Mechi za Kimataifa.

Kilichomkasirisha Rais Magufuli NOVEMBER 9 2015

                                             

Taarifa ya chote kilichotokea mchana wa November 9 2015 na
kumkasirisha Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Dr. Magufuli
kinaelezwa hapa chini na katibu mkuu kiongozi Balozi Ombeni Sefue,
bonyeza play kwenye hii video


               

MATOKEO NA MSIMAMO WA LIGI KUU TANZANIA BARA BAADA YA MICHEZO YA LEO





Ligi kuu Tanzania bara imeendelea leo kwa michezo mitatu katika miji mitatu tofauti.Jiji Dar es salaam kulikua na mchezo mmoja katika uwanja wa Chamazi Wenyeji Azam Fc wameshinda 5-0 dhidi ya Toto Africans,Jiji Tanga African wana kimanu manu wamekubali kulala goli 0-2 nyumbani dhidi ya vibonde JKT Ruvu walioshinda mchezo wao wa kwanza leo.Nako jiji Mbeya Wajerajera wamevutana sharti kwa kufungana magoli 2-2 dhidi ya Ndanda Fc.

Kagame kuiongoza Rwanda hadi 2034?


 

 Bunge la Rwanda limepitisha sheria itakayomruhusu rais Paul Kagame kugombea tena urais kwa mihula miwili. Muhula wa kwanza utakuwa wa miaka saba na unaofuata wa miaka mitano.
Hii kutangazwa kwa uamuzi huu umehitimisha safari ya miezi mitatu iliyoanza mwezi wa saba ambapo bunge la Rwanda lilianza mchakato mchakato wa mabadiliko ya katiba. Akizungumza bungeni baada ya kupitisha uamuzi huo, spika wa bunge la Rwanda Donatille Mukabarisa amesema: "Tumeweka muhula wa miaka saba pekee ambayo unafuata muhula huu unaomalizika na unaozungumziwa kwenye kipengele kilichotangulia. Tumeuweka muhula huu kama wa mpito tu kwa sababu kwa mujibu wa sheria kunapotokea mabadiliko ni lazima kuwepo na kipindi cha kuweka mambo sawa, na hii ni kwa sababu tunataka kuelekea kule tunakopenda."
Katiba ya Rwanda kulingana na nchi za Afrika Mashariki
Uamuzi huo umeridhiwa na wabunge wote 80 wa wabunge la Rwanda lakini mjadala uliochukua muda ni ule kuhusu baadhi ya vipengele vingine hasa kile kinachohusu hatima ya Rais anapostaafu. "Ni lazima tutazame pia mahitaji zaidi kwa rais anayeomba kuwa seneta baada ya kumaliza muhula wake kwa sababu kuwahi kuwa Rais hakupaswi kumpa mtu tiketi ya moja kwa moja ya Rais na hii ni kwa sababu anaweza kuwa alifanya mambo ambayo hayawezi kumruhusu kufanya kazi hiyo ya useneta," amesema mbunge mmoja.
Mabadiliko haya ya katiba yanakwenda mbali na kusema kwamba baada ya muhula huo wa miaka saba Rwanda itaendelea na mihula ya miaka mitano inayompa Rais nafasi kugombea mara mbili tu. Lakini la miaka saba na miaka mitano likaonekana kwuachanganya baadhi ya wananchi.
Spika wa bunge amesema kimsingi wabunge wamepitisha uamuzi huo ili kwamba baadaye katiba ya Rwanda iende sambamba na nchi nyingine za Jumuiya ya Afrika Mashariki hasa kuhusu mihula ya miaka 5 ya urais. Kutokana na mabadiliko haya huenda sasa Rais Paul Kagame akaitawala Rwanda hadi mwaka 2034.

MOURINHO;KUBAKI CHELSEA LICHA VIPIGO MFULULIZO

 MOURINHO-SHINGONI                                                                                                                                    MENEJA wa Chelsea Jose Mourinho atabakia kwenye kibarua chake kwa sasa licha ya Jana kutandikwa 3-1 Uwanjani kwao Stamford Bridge na Liverpool kwenye Mechi ya Ligi Kuu England ikiwa ni ni kipigo chao cha 6 katika Mechi 11 za Ligi hiyo Msimu huu.
Chelsea, ambao ndio Mabingwa Watetezi wa Ligi Kuu England, wapo Nafasi ya 15 kwenye Msimamo wa Ligi wakiwa Pointi 14 nyuma ya Vinara Man City.
Akihojiwa mara baada ya kipigo cha Jana kama anadhani hiyo ndio Mechi yake ya mwisho kama Meneja, Mourinho alijibu: “Hapana. Sifikirii hilo!”
Mourinho, ambae hajawahi kufungwa zaidi ya Mechi 6 za Ligi katika Msimu mmoja akiwa kama Meneja wa Chelsea, aliongeza: “Mapambano yanaendelea lakini wakati mwingine mapambano haya ni magumu kushinda. Unaingia kwenye mapigano na silaha nyingine!”
MATOKEO:
Jumamosi Oktoba 31
Chelsea 1 Liverpool 1       
Crystal Palace 0 Man United 0              
Man City 2 Norwich 1                
Newcastle 0 Stoke 0                  
Swansea 0 Arsenal 3        
Watford 2 West Ham 0               
West Brom 2 Leicester 3   
RATIBA:
**Saa za Bongo
Jumapili Novemba 1
1630 Everton v Sunderland                  
1900 Southampton v Bournemouth                 
Jumatatu Novemba 2
2300 Tottenham v Aston Villa
 BPL-STAND-OCT31

SAMATTA AIPA USHINDI TP MAZEMBE KLABU BINGWA AFRIKA-FAINALI

MAZEMBE                                                                                                                                STRAIKA mahiri wa Tanzania Mbwana Samatta Jana Usiku alifunga Bao la ushindi kwa Klabu yake TP Mazembe ya Congo DR walipocheza Mechi ya Kwanza ya Fainali ya CAF CHAMPIONZ LIGI dihidi ya USM d’Alger huko Algiers na kushinda 2-1.
Bao hilo la Samatta lilifungwa kwa Penati katika ya Dakika ya 79.
TP Mazembe walitangulia kufunga Bao katika Dakika ya 27 kupitia Rainford Kalaba na Mchezaji huyo kutolewa kwa Kadi Nyekundu Dakika ya 45.
Nao USM d’Alger walibaki Mtu 10 kuanzia Dakika ya 67 baada ya Hocine El Orfi kutolewa nje kwa Kadi Nyekundu na Mazembe kupewa Penati ambayo Nathan Sinkala wa Zambia alikosa.
USM d’Alger walisawazisha katika Dakika ya 88 kwa Bao la Mohamed Sequer lakini Mtanzania Mbwana Samatta akaleta ushindi kwa Bao lake la Penati na TP Mazembe kuibuka kidedea kwa Bao 2-1.
Marudiano ya Fainali hii ni Novemba 8 huko Lubumbashi, Congo DR.
Mshindi wa Fainali hizi atazoa Donge la Dola Milioni 1.5 na pia ataiwakilisha Afrika kwenye Mashindano ya FIFA ya Klabu Bingwa Duniani huko Japan Mwezi Desemba.
CAF CHAMPIONZ LIGI
FAINALI
Ratiba/Matokeo:
**Saa za Bongo
Jumamosi Oktoba 31
Union Sportive Medina d’Alger [Algeria] 1 TP Mazembe [Congo, DR] 2
Marudiano
Jumapili Novemba 8
1630 TP Mazembe v Union Sportive Medina d’Alger

Kauli ya kwanza ya Dr. Magufuli baada ya ushindi wa urais na shangwe za ...

 
Baada ya Rais mteule wa Tanzania, Dr. John Magufuli na Makamu wake Mama Samia Suluhu Hassan kukabidhiwa cheti na Tume ya Uchaguzi NEC, safari ilianza toka Ukumbi wa Diamond Jubilee Upanga mpaka Ofisi za CCM mtaa wa Lumumba Dar ambapo wanaCCM na viongozi wengine walikusanyika.
Video yake kwenye kile alichokisema kwenye Jukwaa la CCM mtaa wa Lumumba hiki hapa…

                                                         

CONGRATULATION MY LOVE BROTHER.....

 
Supported by AMAGA Media services : | |
Copyright © 2015. UKURASA WA HABARI - All Rights Reserved
Templete Designed by Abdallah Magana
Proudly powered by Blogger